Wakolosai 2
Neno: Bibilia Takatifu
2 Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Mungu walioko Laodikia, na kwa ajili ya wengine wote ambao hawajapata kuniona. 2 Shabaha yangu ni kuwa wafarijiwe moyoni na kuunganishwa katika upendo, ili wapate uta jiri wa ufahamu kamili, wajue siri ya Mungu, yaani Kristo; 3 ambaye kwake hupatikana hazina yote ya hekima na maarifa. 4 Nawaambia haya ili mtu ye yote asije akawadanganya kwa maneno ya kuvutia. 5 Maana ingawa mimi niko mbali nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi mnaendelea vizuri na kwamba imani yenu katika Kristo ni imara.
Maisha Kamili Katika Kristo
6 Basi, kama mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kuishi ndani yake. 7 Muwe na mizizi ndani yake, na kujengwa juu yake; mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa na kububu jika kwa shukrani.
8 Angalieni mtu ye yote asiwateke kwa falsafa duni na potofu ambazo hutegemea mapokeo ya kibinadamu na mafundisho ya kidunia, na wala si Kristo mwenyewe. 9 Maana, ukamilifu wote wa kimungu umo ndani ya Kristo katika umbile lake la kibinadamu. 10 Nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye yeye ni mkuu juu ya kila uwezo na kila mamlaka. 11 Katika Kristo mmetahiriwa kwa kuondolewa hali yenu ya asili ya dhambi. Hii si tohara inayofa nywa kwa mikono ya binadamu bali inafanywa na Kristo. 12 Mli zikwa pamoja naye katika ubatizo na kufufuliwa pamoja naye kwa kuamini uweza wa Mungu aliyemfufua kutoka kwa wafu.
13 Mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya dhambi zenu na kwa sababu ya kutotahiriwa kwa hali yenu ya asili ya dhambi, Mungu aliwafa nya hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote, 14 baada ya kufuta kabisa hati ya mashtaka iliyokuwa inatukabili na kutu pinga pamoja na masharti yake; aliiondoa akaipigilia msalabani. 15 Na baada ya kuvunja nguvu na mamlaka ya shetani, Mungu alim fedhehesha hadharani kwa kuonyesha ushindi wa msalaba juu yake.
16 Kwa hiyo msimruhusu mtu awahukumu kuhusu chakula au kiny waji, au juu ya kuadhimisha sherehe za dini, sikukuu ya mwezi mpya au siku ya sabato. 17 Maana hizi zilikuwa ni kanuni za muda tu au vivuli vya yale mambo ambayo yangekuja; lakini hakika ya mambo yenyewe ni Kristo. 18 Msikubali kuhukumiwa na mtu ye yote anayejifanya mnyenyekevu na asemaye kwamba ni lazima kuabudu mal aika, mkapoteza tuzo yenu. Mtu kama huyo hufurahia kueleza kwa kirefu maono aliyoona na mawazo yake yasiyo ya kiroho humfanya awe na kiburi. 19 Mtu kama huyo amepoteza uhusiano na Kristo ambaye ni kichwa ambacho kimeunganika na mwili wote na kushika manishwa pamoja kwa mishipa yake na kukua kama Mungu apendavyo.
Kufa Na Kuishi Pamoja Na Kristo
20 Ikiwa mmekufa pamoja na Kristo na hamtawaliwi tena na kanuni za dunia hii, kwa nini bado mnaishi kana kwamba bado mna tawaliwa na masharti ya kidunia? 21 “Usishike hiki! Usionje hiki! Usiguse hiki!” 22 Masharti haya yote hayana budi kuteke tea kwa sababu yanatokana na sheria na mafundisho ya binadamu. 23 Masharti yenyewe yanaonekana kuwa ni ya hekima, maana yana jiwekea namna zake za ibada, unyenyekevu bandia na kuuadhibu mwili. Lakini hayana uwezo wo wote kuzuia tamaa za mwili.
Colossians 2
New International Version
2 I want you to know how hard I am contending(A) for you and for those at Laodicea,(B) and for all who have not met me personally. 2 My goal is that they may be encouraged in heart(C) and united in love, so that they may have the full riches of complete understanding, in order that they may know the mystery(D) of God, namely, Christ, 3 in whom are hidden all the treasures of wisdom and knowledge.(E) 4 I tell you this so that no one may deceive you by fine-sounding arguments.(F) 5 For though I am absent from you in body, I am present with you in spirit(G) and delight to see how disciplined(H) you are and how firm(I) your faith in Christ(J) is.
Spiritual Fullness in Christ
6 So then, just as you received Christ Jesus as Lord,(K) continue to live your lives in him, 7 rooted(L) and built up in him, strengthened in the faith as you were taught,(M) and overflowing with thankfulness.
8 See to it that no one takes you captive through hollow and deceptive philosophy,(N) which depends on human tradition and the elemental spiritual forces[a] of this world(O) rather than on Christ.
9 For in Christ all the fullness(P) of the Deity lives in bodily form, 10 and in Christ you have been brought to fullness. He is the head(Q) over every power and authority.(R) 11 In him you were also circumcised(S) with a circumcision not performed by human hands. Your whole self ruled by the flesh[b](T) was put off when you were circumcised by[c] Christ, 12 having been buried with him in baptism,(U) in which you were also raised with him(V) through your faith in the working of God, who raised him from the dead.(W)
13 When you were dead in your sins(X) and in the uncircumcision of your flesh, God made you[d] alive(Y) with Christ. He forgave us all our sins,(Z) 14 having canceled the charge of our legal indebtedness,(AA) which stood against us and condemned us; he has taken it away, nailing it to the cross.(AB) 15 And having disarmed the powers and authorities,(AC) he made a public spectacle of them, triumphing over them(AD) by the cross.[e]
Freedom From Human Rules
16 Therefore do not let anyone judge you(AE) by what you eat or drink,(AF) or with regard to a religious festival,(AG) a New Moon celebration(AH) or a Sabbath day.(AI) 17 These are a shadow of the things that were to come;(AJ) the reality, however, is found in Christ. 18 Do not let anyone who delights in false humility(AK) and the worship of angels disqualify you.(AL) Such a person also goes into great detail about what they have seen; they are puffed up with idle notions by their unspiritual mind. 19 They have lost connection with the head,(AM) from whom the whole body,(AN) supported and held together by its ligaments and sinews, grows as God causes it to grow.(AO)
20 Since you died with Christ(AP) to the elemental spiritual forces of this world,(AQ) why, as though you still belonged to the world, do you submit to its rules:(AR) 21 “Do not handle! Do not taste! Do not touch!”? 22 These rules, which have to do with things that are all destined to perish(AS) with use, are based on merely human commands and teachings.(AT) 23 Such regulations indeed have an appearance of wisdom, with their self-imposed worship, their false humility(AU) and their harsh treatment of the body, but they lack any value in restraining sensual indulgence.
Footnotes
- Colossians 2:8 Or the basic principles; also in verse 20
- Colossians 2:11 In contexts like this, the Greek word for flesh (sarx) refers to the sinful state of human beings, often presented as a power in opposition to the Spirit; also in verse 13.
- Colossians 2:11 Or put off in the circumcision of
- Colossians 2:13 Some manuscripts us
- Colossians 2:15 Or them in him
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.