Add parallel Print Page Options

Mpango wa Kumwua Yesu

(Mk 14:1-2; Lk 22:1-2; Yh 11:45-53)

26 Yesu alipomaliza akasema haya yote, akawaambia wafuasi wake, “Mnajua kuwa kesho kutwa ni Pasaka. Siku hiyo Mwana wa Adamu atakabidhiwa kwa maadui zake ili auawe msalabani.”

Ndipo viongozi wa makuhani na wazee walikutana katika nyumba ya Kayafa kuhani mkuu. Katika mkutano huo walitafuta njia ya kumkamata na kumwua Yesu kwa siri pasipo mtu yeyote kujua. Wakasema, “Hatuwezi kumkamata Yesu wakati wa sherehe ya Pasaka. Hatutaki watu wakasirike na kusababisha vurugu.”

Mwanamke Ampa Yesu Heshima

(Mk 14:3-9; Yh 12:1-8)

Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni aliyekuwa na ugonjwa mbaya sana wa ngozi. Mwanamke alimwendea, akiwa na chupa yenye manukato ya thamani kubwa. Yesu akiwa anakula, mwanamke huyo akamwagia manukato hayo kichwani.

Wanafunzi walipomwona mwanamke akifanya hivi walimkasirikia. Walisema, “Kwa nini kuharibu manukato hayo? Yangeuzwa na pesa nyingi ingepatikana, na pesa hiyo wangepewa maskini.”

10 Lakini Yesu alijua kilichokuwa kinaendelea. Akasema, “Kwa nini mnamsumbua mwanamke huyu? Amenifanyia jambo zuri sana. 11 Mtaendelea kuishi na maskini siku zote.[a] Lakini ninyi hamtakuwa nami siku zote. 12 Mwanamke huyu amenimwagia manukato. Amefanya hivi kuniandaa kwa ajili ya mazishi baada ya kufa. 13 Habari Njema itahubiriwa kwa watu wote ulimwenguni. Na ninaweza kuwathibitishia kuwa kila mahali ambako Habari Njema zitahubiriwa, jambo alilofanya mwanamke huyu litahubiriwa pia, na watu watamkumbuka.”

Yuda Akubali Kuwasaidia Adui wa Yesu

(Mk 14:10-11; Lk 22:3-6)

14 Ndipo Yuda Iskariote, mmoja wa wanafunzi kumi na wawili wa Yesu alikwenda kuzungumza na wakuu wa makuhani. 15 Akasema, “Nikimkabidhi Yesu kwenu, mtanilipa nini?” Makuhani walimpa sarafu thelathini za fedha. 16 Kuanzia siku hiyo, Yuda alianza kutafuta muda mzuri wa kumsaliti Yesu.

Karamu ya Pasaka

(Mk 14:12-21; Lk 22:7-14,21-23; Yh 13:21-30)

17 Ilipofika siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wafuasi wake walimjia Yesu na kumwambia, “Tutaandaa kila kitu kwa ajili yako ili ule mlo wa Pasaka. Unataka tuandae wapi mlo wa Pasaka?”

18 Yesu akajibu, “Nendeni mjini kwa mtu ninayemfahamu. Mwambieni kuwa Mwalimu anasema, ‘Muda uliowekwa kwa ajili yangu umekaribia sana. Mimi na wafuasi wangu tutakula mlo wa Pasaka katika nyumba yako.’” 19 Walitii na kufanya kama Yesu alivyowaambia. Waliandaa mlo wa Pasaka.

20 Jioni ilipowadia, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili. 21 Walipokuwa wakila Yesu akasema, “Niaminini, ninapowaambia kuwa mmoja wenu ninyi kumi na wawili atanikabidhi kwa maadui zangu.”

22 Wanafunzi walisikitika sana waliposikia hili. Kila mmoja akasema, “Bwana, hakika si mimi!”

23 Yesu akajibu, “Yeye aliyechovya mkate wake katika kikombe kile kile nilichochovya mimi ndiye atakayenisaliti. 24 Mwana wa Adamu atakiendea kifo chake kama Maandiko yanavyosema. Lakini ole wake mtu yule anayemsaliti Mwana wa Adamu ili auawe. Ni bora mtu huyo asingezaliwa.”

25 Ndipo Yuda, ambaye ndiye angemsaliti, akamwambia Yesu, “Mwalimu, hakika si mimi unayemzungumzia, ama ndiye?”

Yesu akamjibu, “hicho ndicho unachosema.”

Chakula cha Bwana

(Mk 14:22-26; Lk 22:15-20; 1 Kor 11:23-25)

26 Walipokuwa wakila, Yesu alichukua baadhi ya mikate na akamshukuru Mungu. Alimega baadhi ya vipande, akawapa wafuasi wake na akasema, “Chukueni mkate huu na mle. Ni mwili wangu.”

27 Kisha akachukua kikombe chenye divai, akamshukuru Mungu na akawapa. Akasema, “Kila mmoja wenu anywe divai iliyo katika kikombe hiki. 28 Divai hii ni damu yangu, itakayomwagika ili kusamehe dhambi za watu wengi na kuanza Agano Jipya ambalo Mungu analifanya na watu wake. 29 Ninataka mjue kuwa, hii ni mara ya mwisho nitakunywa divai mpaka siku ile nitakapokunywa divai mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”

30 Waliimba wimbo kwa pamoja kisha wakaenda kwenye Mlima wa Mizeituni.

Yesu Asema Wafuasi Wake Watamwacha

(Mk 14:27-31; Lk 22:31-34; Yh 13:36-38)

31 Yesu akawaambia wafuasi wake, “Usiku wa leo ninyi nyote mtapoteza imani yangu kwangu. Maandiko yanasema,

‘Nitamwua mchungaji,
    na kondoo watatawanyika.’(A)

32 Lakini baada ya kuuawa, nitafufuka Kisha nitakwenda Galilaya. Nitakuwa huko kabla ninyi hamjaenda huko.”

33 Petro akajibu, “Wafuasi wengine wote wanaweza kupoteza imani juu yako. Lakini imani yangu haitatetereka.”

34 Yesu akajibu, “Ukweli ni huu, usiku wa leo utasema haunifahamu. Utanikana mara tatu kabla jogoo hajawika.”

35 Lakini Petro akajibu, “Sitasema kwamba sikufahamu! Mimi hata nitakufa pamoja nawe!” Na wafuasi wengine wote wakasema kitu hicho hicho.

Yesu Aomba Akiwa Peke Yake

(Mk 14:32-42; Lk 22:39-46)

36 Kisha Yesu akaondoka pamoja na wafuasi wake na kwenda mahali panapoitwa Gethsemane. Akawaambia, “Kaeni hapa wakati ninakwenda mahali pale kuomba.” 37 Alimwambia Petro na wana wawili wa Zebedayo waende pamoja naye. Kisha akaanza kuhuzunika na kuhangaika. 38 Yesu akamwambia Petro na wana wa Zebedayo, “Moyo wangu ni mzito na wenye huzuni hata kujisikia kana kwamba huzuni hiyo itaniua. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”

39 Kisha Yesu akaenda mbele kidogo. Akainama hadi chini uso wake ukiigusa nchi akiomba na akasema, “Baba yangu, ikiwezekana, usifanye nikinywee kikombe hiki cha mateso.[b] Lakini fanya lile ulitakalo na si lile ninalolitaka mimi.” 40 Kisha akarudi walipokuwa wafuasi wake na akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Je hamkuwa na uwezo wa kukesha pamoja nami hata kwa saa moja? 41 Amkeni kesheni na kuomba ili muyashinde majaribu. Roho zenu zinataka kufanya mambo sahihi, lakini miili yenu ni dhaifu.”

42 Kisha Yesu akaenda mara ya pili na akaomba akisema, “Baba yangu, ikiwa ni lazima nikinywee kikombe hiki na haiwezekani nikakwepa, basi mapenzi yako na yatimizwe.”

43 Kisha akarudi na kwenda walipokuwa wafuasi wake, akawakuta wamelala tena. Hawakuweza kukesha. 44 Hivyo akawaacha akaenda tena kuomba. Mara hii ya tatu alipokuwa anaomba akasema kama alivyosema hapo mwanzo.

45 Kisha Yesu akawarudia wafuasi wake na akasema, “Bado mnalala na kupumzika? Wakati wa Mwana wa Adamu kukabidhiwa kwa wenye dhambi umewadia. 46 Simameni! Tuondoke. Tazama yeye atakayenikabidhi anakuja.”

Yesu Akamatwa

(Mk 14:43-50; Lk 22:47-53; Yh 18:3-12)

47 Yesu alipokuwa anazungumza, Yuda mmoja wa wanafunzi wake kumi na mbili alifika akiwa na kundi kubwa la watu, waliokuwa wamebeba majambia na marungu. Walikuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu. 48 Yuda aliyekuwa amkabidhi Yesu kwao, alipanga kufanya kitu cha kuwajulisha yupi kati ya wafuasi alikuwa Yesu. Alisema, “Mtu nitakayembusu ndiye mtakayemkamata.” 49 Hivyo Yuda alikwenda kwa Yesu na kumwambia, “Salamu, Mwalimu!” Kisha akambusu.

50 Yesu akajibu, “Rafiki yangu, fanya ulilokuja kufanya.”

Kisha wale watu wakaja na kumkamata Yesu. 51 Jambo hili lilipotokea, mmoja wa wafuasi wa Yesu alichukua jambia lake na kumkata sikio mtumishi wa kuhani mkuu.

52 Yesu akamwambia, “Rudisha jambia lako mahali pake. Atumiaye jambia atauawa kwa jambia. 53 Hakika unajua kuwa ningemwomba Baba yangu yeye angenipa zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika. 54 Lakini hilo lisingekubaliana na yale Maandiko, yanayosema hivi ndivyo ilivyopasa itokee.”

55 Kisha Yesu akaliambia kundi, “Kwa nini mnakuja kunikamata mkiwa na mikuki na marungu kama vile mimi ni mhalifu? Nimekuwa nakaa eneo la Hekalu nikifundisha kila siku. Kwa nini hamkunikamata kule? 56 Lakini mambo haya yote yametokea ili kutimiza Maandiko yaliyoandikwa na manabii.” Ndipo wafuasi wake wote wakamwacha na kukimbia.

Yesu Akiwa Mbele ya Viongozi wa Kidini

(Mk 14:53-65; Lk 22:54-55,63-71; Yh 18:13-14,19-24)

57 Wale waliomkamata Yesu wakampeleka nyumbani kwa Kayafa, kuhani mkuu. Walimu wa Sheria na viongozi wazee wa Kiyahudi walikuwa wamekusanyika huko. 58 Petro alimfuata Yesu lakini alikuwa mbali kidogo. Alimfuata mpaka katika ua wa nyumba ya kuhani mkuu. Petro alienda uani na akakaa pamoja na walinzi. Alitaka kuona nini kingetokea.

59 Viongozi wa makuhani na baraza kuu walijaribu kutafuta kosa ili waweze kumwua Yesu. Walijaribu kutafuta watu ili wadanganye kuwa Yesu alifanya kosa. 60 Watu wengi walikuja na akasema uongo kuhusu Yesu. Lakini baraza lilishindwa kupata ushahidi wa kuutumia ili kumwua. Ndipo watu wawili walikuja 61 na akasema, “Mtu huyu[c] alisema, ‘Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”

62 Kisha kuhani mkuu alisimama na kumwambia Yesu, “Huna neno lolote la kujitetea dhidi ya mashtaka haya juu yako? Wanasema kweli?” 63 Lakini Yesu hakusema neno lolote.

Kisha kuhani mkuu akamwambia Yesu, “Apa mbele za Mungu aliye hai kwamba utatuambia kweli. Je, wewe ni Masihi, Mwana wa Mungu?”

64 Yesu akajibu, “Unaweza akasema hivyo, Mimi ndiye. Lakini ninawaambia, kitambo kidogo mtamwona Mwana wa Adamu akiwa amekaa upande wa kuume wa Mungu, mwenye Nguvu. Na mtamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni.”

65 Kuhani mkuu aliposikia hili, alilarua vazi lake kwa hasira. Akasema, “Mtu huyu amemtukana Mungu! Hatuhitaji mashahidi zaidi. Ninyi nyote mmesikia matusi yake. 66 Mnasemaje?”

Viongozi wa Kiyahudi wakajibu, “Ana hatia, na ni lazima afe.”

67 Na baadhi ya waliokuwa pale wakamtemea mate Yesu usoni na kumpiga makonde na wengine walimpiga makofi. 68 Wakasema, “Tuonyeshe kuwa wewe ni nabii, Masihi! Nani amekupiga!”

Petro Amkana Yesu

(Mk 14:66-72; Lk 22:56-62; Yh 18:15-18,25-27)

69 Petro alipokuwa amekaa nje uani, msichana mtumishi akamwendea. Akasema, “Ulikuwa pamoja na Yesu, yule mtu kutoka Galilaya.”

70 Lakini Petro akamwambia kila mtu aliyekuwa pale kuwa si kweli. Akasema “Sijui unachosema.”

71 Kisha akaondoka uani. Akiwa kwenye lango msichana mtumishi akamwona na akawaambia watu waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”

72 Kwa mara nyingine tena Petro akasema hakuwa pamoja na Yesu. Akasema, “Ninaapa kwa Mungu, simfahamu mtu huyu!”

73 Baada ya muda mfupi baadaye, watu waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro na kumwambia, “Tunajua wewe ni mmoja wao. Hata namna unavyoongea inaonesha wazi kuwa ndivyo hivyo.”

74 Kisha Petro akaanza kujiapiza mwenyewe ikiwa anaongopa. Akasema, “Ninaapa kwa Mungu, simfahamu mtu huyu!” Mara alipomaliza akasema hili, jogoo akawika. 75 Kisha akakumbuka maneno alivyoambiwa na Yesu kuwa: “Kabla jogoo hajawika, utakuwa umenikana mara tatu.” Kisha Petro akatoka nje na kulia kwa uchungu sana.

Footnotes

  1. 26:11 Mtaendelea kuishi na maskini siku zote Tazama Kum 15:11.
  2. 26:39 kikombe Kikombe ni ishara ya mateso. Yesu alitumia dhana ya kukinywea kikombe akimaanisha kuyakubali mateso ambayo angeyapata katika matukio ya kutisha ambayo yangetokea muda mfupi ujao.
  3. 26:61 Mtu huyu Yaani, Yesu. Adui zake walikuwa wanakwepa kutamka jina lake.

26 And it came about when Rebbe, Melech HaMoshiach completed all these divrei torah, he said to his talmidim,

You know, that after two days, there is Pesach, and the Ben HaAdam is handed over for talui al HaEtz (DEVARIM 21:23; DANIEL 7:13).

Then the Rashei Hakohanim and the Ziknei haAm (Elders of the People) were assembled in the courtyard of the residence of the Kohen Gadol (High Priest), the one being called Caiapha.

And they planned to arrest Yeshoshua by a trap and kill him.

But they were saying, Not during the Chag (Feast), lest a riot break out among the am haaretz. [T.N. A careful reading of this book shows that the Moshiach pointed to the One in Ps 110:1, Dan 7:13, and Isa 53 and Ps 118:22 and declared that the same person is being referred to in all these Scriptures: Moshiach Adoneinu.]

And, while Rebbe, Melech HaMoshiach was in Beit-Anyah in the bais of Shimon the leper,

An isha approached him with an alabaster flask of costly perfume, and she poured it out on Moshiach’s rosh, as he sat bimesibba (reclining at tish [table]).

And having seen this, Moshiach’s talmidim were angry, saying, For what is this waste?

For it would have been possible to sell this for a generous sum and give to the aniyim (poor ones).

10 Aware of this, Rebbe, Melech HaMoshiach said to them, Why are you bringing about difficulty for the isha for the ma’aseh tov (good deed) she does to me.

11 For the aniyim you have with you always, but you do not always have me.

12 For this isha (woman) has poured this ointment on my basar (body) in order to prepare me for kevurah (burial). [Isa 53:9 Ps 16:9-10]

13 Omein, I say to you, wherever this Besuras HaGeulah is preached bchol HaOlam (in all the world), in her memory it will be spoken also what was done by her.

14 Then, one of the Shneym Asar (Twelve), Yehudah from Kriot, went to the Rashei Hakohanim

15 and said, What are you willing to give me? And I will hand him over to you. And they weighed out for him sheloshim shiklei kesef (thirty pieces of silver).

16 And from then on he was seeking an opportunity that he might hand Rebbe, Melech HaMoshiach over.

17 But at the onset of Chag HaMatzot, Moshiach’s talmidim approached him, saying, Where do you wish we should prepare for you your Seder?

18 And he said, Go into the city to such and such person and say to him, Our Rebbe says, My time is at hand. With you I am observing Pesach with my talmidim.

19 And the talmidim did as Rebbe, Melech HaMoshiach commanded them, and they prepared the Seder.

20 When erev came, Rebbe, Melech HaMoshiach was sitting bimesibba (reclining) at tish with the Shneym Asar Talmidim.

21 And as they were eating with their Rebbe, he said, Omein, I say to you that one of you will be my betrayer.

22 And much distressed, each one began to say to him, Surely I am not the one, Adoni?

23 But, in reply, he said, The one having dipped the hand into the bowl [SHEMOT 12:8] with me, this one is my betrayer.

24 Indeed the Ben Adam [Moshiach] goes as it was written concerning him, but oy to that man through whom the Ben HaAdam is betrayed. It would have been better for that man if he had not been born.

25 And, in reply, Yehudah the betrayer of Rebbe, Melech HaMoshiach, said, Surely I am not the one, Rabbi? Moshiach says to Yehudah, You have said it.

26 And at the Seudah, Rebbe, Melech HaMoshiach, having taken matzah, having made HaMotzi, he broke the [middle] matzah, giving the afikoman to the talmidim, and said, Take and eat, this is my basar.

27 And having taken the Cup of Redemption and having made the bracha, he gave it to them, saying, Drink from it, all of you.

28 For this is my [Moshiach’s, see Isa 53:7-8] Dahm HaBrit HaChadasha [Isa 42:6; Jer 31:31-34], which is poured out LARABBIM (for many YESHAYAH 53:11-12) for the selicha (forgiveness) of chattaim (sins).

29 And I say to you, I will by no means drink from now on of this pri hagefen (fruit of the vine) until that Day when I drink it with you chadash (new) in the Malchut Avi.

30 And having sung the Hallel, they went out to the Har HaZeytim.

31 Then Rebbe, Melech HaMoshiach says to them, All of you will be offended at me [Moshiach] during this night, for it has been written, HACH ES HAROEH UTEFUTSEN HATSON (Strike the Shepherd and the sheep will be scattered ZECHARYAH 13:7).

32 But after I undergo Techiyas HaMoshiach I will go ahead of you to the Galil. [Mt 28:7]

33 And, in reply, Kefa said to him, If everyone will be offended at you, I never will be offended.

34 He said to him, Omein, I say to you that balailah hazeh (during this night), before a tarnegol (cock) crows, you will make hakhchashah (denial) of me [as Moshiach] shalosh paamim (three times).

35 Kefa says to him, Even if it is necessary for me to die al kiddush ha-Shem with you, by no means will I deny you. Likewise all the talmidim spoke also.

36 Then Rebbe, Melech HaMoshiach comes with them to a place being called Gat-Shmanim, and Rebbe, Melech HaMoshiach says to the talmidim, Sit here until I go over there and daven.

37 And having taken Kefa and the two sons of Zavdai, Rebbe, Melech HaMoshiach began to be sorrowful and distressed with agmat nefesh (grief).

38 Then he says to them, My nefesh is deadly grieved, even to the point of mavet. Remain here and stay awake with me.

39 And having gone forward a short distance, Rebbe, Melech HaMoshiach fell upon his face, davening and saying, Avi, if it is possible, let this Kos pass from me. But not as I will, but as you will (Mt 6:10; 12:50).

40 Then he comes to the talmidim and finds them sleeping, and he says to Kefa, So were you not strong enough to be awake for one hour with me?

41 Stay awake and offer tefillos, lest you enter lidey nisayon (Mt 6:13). Indeed the ruach is willing but the basar is weak.

42 Again, for a second time, having left, he davened, saying, Avi, if it is not possible for this to pass by except I drink it, let yeaseh rtzonechah (your will be done). [Mt 6:10]

43 And having come again, Rebbe, Melech HaMoshiach found the talmidim sleeping, for their eyes were too heavy to stay open.

44 And having left them again and having gone away, he was davening for the shlishit (third) time, saying the same words.

45 Then he comes to the talmidim and says to them, Sleep on now and take your rest. Hinei! The hour is at hand, and the Ben HaAdam Rebbe Melech HaMoshiach is being betrayed into the hands of choteim (sinners).

46 Arise, and let us go. Hinei! My betrayer has drawn near.

47 And while he was still speaking hinei! Yehudah, one of the Shneym Asar, came and with him came a great multitude with swords and clubs from the Rashei Hakohanim (Chief Priests) and the Ziknei HaAm (the Elders of the People).

48 Now the betrayer had given them a signal, saying, Whomever I may give the neshikah (kiss), he is the one. Chap (grab) him!

49 And immediately, he approached Rebbe, Melech HaMoshiach, and said, Shalom, Rebbe. And he gave him the neshikah.

50 And Rebbe, Melech HaMoshiach said to him, Chaver, do what you came for. Then, having approached, they laid hands on Rebbe, Melech HaMoshiach and arrested him.

51 And hinei! One of the ones with him stretched out his hand, drew his cherev, and struck the servant of the Kohen Gadol, cutting off his ear.

52 Then Rebbe, Melech HaMoshiach says to him, Return your cherev into its place; for all who take the sword will die by the sword.

53 Or do you think that I am not able to call upon Avi, and He will provide me now more than Shneym Asar legions of malachim?

54 But how then may the Kitvei Hakodesh be fulfilled that say it must happen thus?

55 At that moment, he said to the crowd, Do you have the chutzpah (nerve) to come out, as against a revolutionary, with swords and clubs to arrest me? Daily in the Beis Hamikdash I was sitting saying my shiurim and you did not arrest me.

56 But this all happened that the Kitvei Hakodesh of the Neviim might be fulfilled. Then the talmidim deserted Rebbe, Melech HaMoshiach and fled.

57 But the ones having arrested Rebbe, Melech HaMoshiach led him away to Caiapha the Kohen Gadol, where the Sofrim and the Zekenim (Elders) were gathered together.

58 And Kefa was following Rebbe, Melech HaMoshiach from far away. He followed him as far as the courtyard of the Kohen Gadol and, having gone inside it, Kefa was sitting down with the servants to see the maskana (outcome).

59 And the Rashei Hakohanim and the Sanhedrin all were seeking edut sheker (false testimony of false witnesses) against Yehoshua so that they might put him to death.

60 And they found none, though many shakranim (liars) came forward. At last, two came forward

61 and said, This one said, I am able to bring about a churban (destruction) of the Beis Hamikdash of Hashem and within shloshah yamim to rebuild it.

62 And having got up, the Kohen Gadol said to Rebbe, Melech HaMoshiach, Do you answer nothing? For what do these men give edut (testimony) against you?

63 But Rebbe, Melech HaMoshiach was silent. And the Kohen Gadol said to him, I adjure you by Hashem, Elohim Chayyim, to tell us if you are the Rebbe, Melech HaMoshiach Ben HaElohim.

64 Rebbe, Melech HaMoshiach says to him, You said it. But I say to you, From now on you will see the Ben HaAdam [Moshiach] sitting at the right hand of Gevurah (Power) and his Bias (Coming) will be with ANENEI HASHOMAYIM (clouds of Heaven, DANIEL 7:13-14).

65 Then the Kohen Gadol made the keriah (rending, tearing of his garments), saying, He has committed Chillul Hashem. What further need do we have of edut? Hinei! Now you have heard the Chillul Hashem.

66 What does it seem to you? And, in reply, they said, He is deserving of mishpat mavet, the death penalty.

67 Then they spat into his face and they struck him and they slapped him,

68 saying, Give us a dvar nevuah, Rebbe, Melech HaMoshiach. Who is the one who hit you?

69 Now Kefa was sitting outside in the courtyard. And one maid approached Kefa, saying, And you were with Yehoshua of the Galil!

70 But Kefa denied it before everyone, saying, I do not have daas of what you are saying.

71 And having gone out to the gate, another saw Kefa and says to the bystanders, There! This one was with Yehoshua of Natzeret!

72 And again Kefa denied it with a shevuah (oath), I do not know the man!

73 And after a little while the bystanders came and said to Kefa, Truly also you are one of them, for even your accent gives you away!

74 Then Kefa began to curse and swear, I do not know the man! And immediately a tarnegol (cock) crowed.

75 And Kefa remembered the word which Rebbe, Melech HaMoshiach had said: Before a tarnegol (cock) crows you will deny me shalosh paamim (three times). And Kefa went out and wept bitterly. [T.N. Read the letters of this Kefa on p. 1104-1112, both attested by early Kehillah tradition or manuscript evidence.]