Matayo 2
Neno: Bibilia Takatifu
Wataalamu Wa Nyota Wafika Kumwona Mtoto Yesu
2 Basi Yesu alipozaliwa katika mji wa Betlehemu huko Yudea, wakati wa utawala wa mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka Mashariki walifika Yerusalemu wakawa wakiuliza, 2 kutoka kwao kuhusu wakati kamili ambao ile nyota ilionekana.
3 Mfalme Herode alipopata habari hizi alifadhaika sana na watu wote wa Yerusalemu wakawa na hali ya wasiwasi. 4 Herode akaitisha mkutano wa makuhani wakuu na waandishi, akawataka wamweleze mahali ambapo Kristo angezaliwa.
5 Wakamjibu, “Atazaliwa Betlehemu ya Yudea, kwa maana nabii aliandika hivi kuhusu jambo hili: 6 ‘Nawe Betlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si wa mwisho miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana atatoka mtawala kwako atakayetawala watu wangu Israeli.’ ”
7 Ndipo Herode akawaita wale wataaamu wa nyota kwa siri aka pata uhakikisho 8 Halafu akawatuma Bethlehemu akiwaagiza, “Nendeni mkamtafute huyo mtoto kwa bidii, na mkishampata, mnile tee habari ili na mimi niende kumsujudia.”
9 Baada ya kumsikiliza mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaendelea na safari, na mbele yao wakaiona ile nyota waliyoiona mashariki ikiwatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto. 10 Walipoiona ile nyota walijawa na furaha isiyoelezeka.
11 Walipoingia ndani ya ile nyumba walimwona mtoto na mama yake Mariamu, wakainama chini kwa heshima kubwa wakamwabudu. Kisha wakafungua mikoba yao, wakampa zawadi: dhahabu, uvumba na manemane. 12 Na baada ya kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Her ode , wakarudi makwao kwa kupitia njia nyingine.
Yosefu, Maria Na Mtoto Yesu Wakimbilia Misri
13 Walipokwisha kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Amka, umchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri na mkae huko mpaka hapo nitakapowaambia; kwa maana mfalme Herode ataanza msako wa kumtafuta huyu mtoto ili amwue.” 14 Kwa hiyo akaamka, akamchukua mtoto na mama yake usiku, wakaelekea Misri 15 na wakakaa huko mpaka Herode alipo fariki. Na hivyo likatimia neno alilosema Bwana hupitia nabii: ‘Nilimwita mwanangu kutoka Misri.’
16 Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota wame mdanganya, alikasirika sana, akawatuma watu kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kwenda chini katika mji wa Betlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda ambao wale wataalamu walikuwa wamemhakikishia. 17 Ndipo maneno yaliy osemwa hupitia nabii Yeremia yakatimia kama alivyosema:
18 “Sauti ilisikika huko Rama, kilio cha uchungu na maom bolezo; Raheli akiwalilia wanae; hakukubali kufarijiwa kwa sababu walikuwa wamekufa.”
19 Lakini Herode alipofariki, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto huko Misri, 20 akamwambia, “Amka mchukue mtoto na mama yake, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliotaka kumwua mtoto wamefariki.”
21 Basi Yosefu akaamka, akamchukua mtoto na mama yake wakar udi nchi ya Israeli. 22 Lakini alipopata habari kwamba Arkelao alikuwa akimiliki huko Yudea mahali pa baba yake Herode, aliogopa kwenda huko; na baada ya kuonywa tena katika ndoto, aliondoka akaenda wilaya ya Galilaya. 23 Akaenda kuishi katika mji ulioitwa Nazareti, na hivyo yakatimia yale yaliyosemwa kupitia manabii kwamba, “Ataitwa Mnazareti.”
Matthew 2
King James Version
2 Now when Jesus was born in Bethlehem of Judaea in the days of Herod the king, behold, there came wise men from the east to Jerusalem,
2 Saying, Where is he that is born King of the Jews? for we have seen his star in the east, and are come to worship him.
3 When Herod the king had heard these things, he was troubled, and all Jerusalem with him.
4 And when he had gathered all the chief priests and scribes of the people together, he demanded of them where Christ should be born.
5 And they said unto him, In Bethlehem of Judaea: for thus it is written by the prophet,
6 And thou Bethlehem, in the land of Juda, art not the least among the princes of Juda: for out of thee shall come a Governor, that shall rule my people Israel.
7 Then Herod, when he had privily called the wise men, enquired of them diligently what time the star appeared.
8 And he sent them to Bethlehem, and said, Go and search diligently for the young child; and when ye have found him, bring me word again, that I may come and worship him also.
9 When they had heard the king, they departed; and, lo, the star, which they saw in the east, went before them, till it came and stood over where the young child was.
10 When they saw the star, they rejoiced with exceeding great joy.
11 And when they were come into the house, they saw the young child with Mary his mother, and fell down, and worshipped him: and when they had opened their treasures, they presented unto him gifts; gold, and frankincense and myrrh.
12 And being warned of God in a dream that they should not return to Herod, they departed into their own country another way.
13 And when they were departed, behold, the angel of the Lord appeareth to Joseph in a dream, saying, Arise, and take the young child and his mother, and flee into Egypt, and be thou there until I bring thee word: for Herod will seek the young child to destroy him.
14 When he arose, he took the young child and his mother by night, and departed into Egypt:
15 And was there until the death of Herod: that it might be fulfilled which was spoken of the Lord by the prophet, saying, Out of Egypt have I called my son.
16 Then Herod, when he saw that he was mocked of the wise men, was exceeding wroth, and sent forth, and slew all the children that were in Bethlehem, and in all the coasts thereof, from two years old and under, according to the time which he had diligently inquired of the wise men.
17 Then was fulfilled that which was spoken by Jeremiah the prophet, saying,
18 In Rama was there a voice heard, lamentation, and weeping, and great mourning, Rachel weeping for her children, and would not be comforted, because they are not.
19 But when Herod was dead, behold, an angel of the Lord appeareth in a dream to Joseph in Egypt,
20 Saying, Arise, and take the young child and his mother, and go into the land of Israel: for they are dead which sought the young child's life.
21 And he arose, and took the young child and his mother, and came into the land of Israel.
22 But when he heard that Archelaus did reign in Judaea in the room of his father Herod, he was afraid to go thither: notwithstanding, being warned of God in a dream, he turned aside into the parts of Galilee:
23 And he came and dwelt in a city called Nazareth: that it might be fulfilled which was spoken by the prophets, He shall be called a Nazarene.
Copyright © 1989 by Biblica