Font Size
1 Timotheo 5:8-10
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
1 Timotheo 5:8-10
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
8 Kila mtu atunze watu wa kwao, muhimu sana watunze familia zao. Kama hawatendi hayo watakuwa hawakubaliani na tunayoamini. Watakuwa wabaya kuliko hata asiyeamini.
9 Ili kuongezwa kwenye orodha ya wajane, mwanamke ni lazima awe na umri wa miaka 60 au zaidi, awe aliyekuwa mwaminifu kwa mume[a] wake. 10 Ni lazima ajulikane kwa mema aliyoyafanya: kulea watoto, kukaribisha wageni kwenye nyumba yake, kuwasaidia watu wa Mungu wenye uhitaji,[b] wenye shida, na kutumia maisha yake kufanya wema wa aina zote.
Read full chapterFootnotes
- 5:9 awe aliyekuwa mwaminifu kwa mume “Mwaminifu kwa mume wake” inamaanisha “mwanamke awe na mtu mmoja.” Au aliyeolewa: Misalaba ya wanawake nyakati za Paulo mara nyingi zilitambulisha kwamba walikuwa wameolewa mara moja tu katika maisha yao. Hili lilitafsiriwa kuwa maisha safi ya heshima ya mwanamke au kuheshimika. Maana ya wazi, “mke wa mume mmoja”, inayoweza pia kutafsiriwa, “mke wa mume mmoja” au “aliyeolewa mara moja tu”.
- 5:10 kuwasaidia … uhitaji Kwa maana ya kawaida, “kuosha miguu”, mila ya utamaduni wa karne ya kwanza, kwa sababu watu walivaa viatu vya wazi na kutembea kwenye barabara za vumbi nyingi.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International