Wakolosai 3
Neno: Bibilia Takatifu
Maisha Mapya
3 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, elekezeni mioyo yenu kwenye mambo ya juu, alikokaa Kristo, upande wa kulia wa Mungu. 2 Yafikirini mambo ya juu na siyo mambo ya hapa duniani. 3 Kwa maana ninyi mlikufa, na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo kwa Mungu. 4 Wakati Kristo ambaye ni uzima wetu ataonekana, ndipo na ninyi mtakapoonekana pamoja naye katika utu kufu.
5 Basi, yaangamizeni kabisa mambo yote yanayotokana na asili yenu ya kidunia: uasherati, mawazo machafu, tamaa mbaya, nia mbaya na choyo ambayo ni ibada ya sanamu. 6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja. 7 Ninyi mlikuwa mkitenda mambo haya katika maisha yenu ya zamani. 8 Lakini sasa ni lazima mwa chane kabisa na mambo kama haya: hasira, ghadhabu, nia mbaya, matukano na maneno machafu kutoka vinywani mwenu. 9 Msiambiane uongo kwa maana mmekwisha vua utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake 10 na kuvaa utu upya ambao unaendelea kufanywa upya katika ufahamu ili ufanane na Muumba wake. 11 Katika hali hii hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, mtu aliyesoma na asiyesoma, mtumwa na mtu huru. Bali Kristo ni yote na yumo ndani ya wote. 12 Basi, kwa kuwa ninyi ni wateule wa Mungu, wapendwa na watakatifu, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 13 Vumilianeni na kusameheana kama mtu ana malalamiko kuhusu mwenzake. Sameheni kama Bwana alivyokwisha kuwasamehe. 14 Juu ya haya yote, vaeni upendo ambao unaunganisha mambo haya kuwa kitu kimoja kilicho kikamilifu.
15 Ruhusuni amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena muwe na shukrani. 16 Neno la Kristo lidumu ndani yenu kwa wingi, mki fundisha na na kuonyana katika hekima yote; na huku mkiimba zab uri, nyimbo na tenzi za rohoni na mkiwa na shukrani kwa Mungu mioyoni mwenu. 17 Na lo lote mtakalofanya, ikiwa kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kupitia kwake.
Wajibu Katika Familia
18 Ninyi wake, watiini waume zenu kama inavyopasa katika Bwana. 19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu wala msiwe wakali juu yao. 20 Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hii humpendeza Bwana. 21 Ninyi akina baba msiwachokoze watoto wenu wasije wakakata tamaa.
22 Nanyi watumwa, watiini mabwana wenu wa hapa duniani katika mambo yote; fanyeni hivyo kwa moyo safi mkimwogopa Mungu, na wala si kwa kutafuta upendeleo wakati wanapowatazama. 23 Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana na siyo wanadamu. 24 Kwa maana mnafahamu kwamba mtapokea urithi wenu kwa Bwana kama tuzo yenu.
Colossians 3
New International Version
Living as Those Made Alive in Christ
3 Since, then, you have been raised with Christ,(A) set your hearts on things above, where Christ is, seated at the right hand of God.(B) 2 Set your minds on things above, not on earthly things.(C) 3 For you died,(D) and your life is now hidden with Christ in God. 4 When Christ, who is your[a] life,(E) appears,(F) then you also will appear with him in glory.(G)
5 Put to death,(H) therefore, whatever belongs to your earthly nature:(I) sexual immorality,(J) impurity, lust, evil desires and greed,(K) which is idolatry.(L) 6 Because of these, the wrath of God(M) is coming.[b] 7 You used to walk in these ways, in the life you once lived.(N) 8 But now you must also rid yourselves(O) of all such things as these: anger, rage, malice, slander,(P) and filthy language from your lips.(Q) 9 Do not lie to each other,(R) since you have taken off your old self(S) with its practices 10 and have put on the new self,(T) which is being renewed(U) in knowledge in the image of its Creator.(V) 11 Here there is no Gentile or Jew,(W) circumcised or uncircumcised,(X) barbarian, Scythian, slave or free,(Y) but Christ is all,(Z) and is in all.
12 Therefore, as God’s chosen people, holy and dearly loved, clothe yourselves(AA) with compassion, kindness, humility,(AB) gentleness and patience.(AC) 13 Bear with each other(AD) and forgive one another if any of you has a grievance against someone. Forgive as the Lord forgave you.(AE) 14 And over all these virtues put on love,(AF) which binds them all together in perfect unity.(AG)
15 Let the peace of Christ(AH) rule in your hearts, since as members of one body(AI) you were called to peace.(AJ) And be thankful. 16 Let the message of Christ(AK) dwell among you richly as you teach and admonish one another with all wisdom(AL) through psalms,(AM) hymns, and songs from the Spirit, singing to God with gratitude in your hearts.(AN) 17 And whatever you do,(AO) whether in word or deed, do it all in the name of the Lord Jesus, giving thanks(AP) to God the Father through him.
Instructions for Christian Households(AQ)
18 Wives, submit yourselves to your husbands,(AR) as is fitting in the Lord.
19 Husbands, love your wives and do not be harsh with them.
20 Children, obey your parents in everything, for this pleases the Lord.
21 Fathers,[c] do not embitter your children, or they will become discouraged.
22 Slaves, obey your earthly masters in everything; and do it, not only when their eye is on you and to curry their favor, but with sincerity of heart and reverence for the Lord. 23 Whatever you do, work at it with all your heart, as working for the Lord, not for human masters, 24 since you know that you will receive an inheritance(AS) from the Lord as a reward.(AT) It is the Lord Christ you are serving. 25 Anyone who does wrong will be repaid for their wrongs, and there is no favoritism.(AU)
Footnotes
- Colossians 3:4 Some manuscripts our
- Colossians 3:6 Some early manuscripts coming on those who are disobedient
- Colossians 3:21 Or Parents
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.